Waraka wa Paulo kwa Waefeso, ni moja ya barua za muhimu sana katika Biblia-Agano Jipya. Katika waraka huu, Mtume Paulo anaelezea kwa undani jinsi Mungu alivyowafanya Wamataifa na Wayahudi kuwa kitu kimoja katika Kristo. Anafunua siri kuu ya ukombozi na kuonesha kwamba watu wote, yaani Wayahudi na wasio Wayahudi ni sawa mbele za Mungu na kwamba wote wanaokolewa kwa neema kwa njia ya imani. Kupitia kwa Yesu Kristo, wote ni watoto wa Mungu na wote ni wenyeji katika maskani yake. Ujumbe wa Paulo katika waraka huu, umeifanya Habari Njema ya wokovu, kuwa Habari Njema kweli kweli. Mwandishi wa kitabu hiki, Mchungaji Christopher Mwashinga, ameelezea sura tatu za kwanza za Waraka huu, kwa namna rahisi, fungu kwa fungu, na kufanya ujumbe wa Paulo ueleweke kwa msomaji yeyote bila kujali kiwango chake cha elimu.
ThriftBooks sells millions of used books at the lowest
everyday prices. We personally assess every book's quality and offer rare, out-of-print treasures. We
deliver the joy of reading in recyclable packaging with free standard shipping on US orders over $15.
ThriftBooks.com. Read more. Spend less.