Skip to content
Scan a barcode
Scan
Paperback Tungo Zetu: Msingi wa Mashairi na Tungo Nyinginezo [Swahili] Book

ISBN: 1399933655

ISBN13: 9781399933650

Tungo Zetu: Msingi wa Mashairi na Tungo Nyinginezo [Swahili]

Wataalamu wa lugha na fasihi na mila za watu mbalimbali wametuzindua juu ya utajiri wa fasihi ya Waswahili. Katika fasihi hiyo, tungo za Kiswahili ndilo jambo lililojitokeza mbele kwa mwanga wenye kunawiri sana. Profesa Ibrahim Noor Shariff amefanya utafiti mkubwa kabla ya kukiandika kitabu hiki. Natija yake ni kuwa yaliyoelezwa humu yametufunulia mengi yaliyokuwa dafina. Tokea 1988 kilipochapishwa kitabu hiki kwa mara ya kwanza kimekuwa ni kitabu cha kukirejelea kwani kinaeleza yale ambayo watungaji wa tungo za Kiswahili, wataalamu, waalimu na wanafunzi wanaotaka kuelewa khabari za tungo huwa wanakirejelea mara kwa mara ili kupata jawabu za masuala yao.


Kitabu hiki kimepangwa vizuri sana kwani kila maudhui yameandikwa chini ya kichwa cha khabari kinachoelezea maudhui yanayofuata. Hali kadhalika, kitabu kina mifano ya tungo za kupigiwa mifano. Yoyote anayetaka kuzungumza khabari za tungo za Waswahili hataweza tena kujadili mengi ya maana iwapo atajinyima fursa ya kusoma yaliyoandikwa katika kitabu hiki cha Tungo Zetu.

Recommended

Format: Paperback

Condition: New

$22.81
Ships within 2-3 days
Save to List

Customer Reviews

0 rating
Copyright © 2026 Thriftbooks.com Terms of Use | Privacy Policy | Do Not Sell/Share My Personal Information | Cookie Policy | Cookie Preferences | Accessibility Statement
ThriftBooks ® and the ThriftBooks ® logo are registered trademarks of Thrift Books Global, LLC
GoDaddy Verified and Secured