Kitabu hiki kimeandikwa kwa kuwalenga watu wa ndani ya nchi na wageni wanaokijua Kiingereza vizuri, lakini, wana hamu/wanahitaji kujua Kiswahili. Lugha hii kwa sasa inazungumzwa na zaidi ya watu milioni 140 duniani. Lakini, hata watu wanaokijua Kiswahili, wanakihitaji kitabu hiki, ili, na wao waweze kuandika na kuzungumza Kiswahili sanifu. Kumbuka kwamba si kila mtu anayezungumza, anayeongea na kuandika Kiswahili, anajua lugha hii kwa ufasaha. Kitabu hiki kitawasaidia watu kuongea na kuandika Kiswahili fasaha. Aidha, kitabu hiki kitawaongezea msamiati wa Kingereza watu wanaojua Kiswahili, lakini, hawajui maneno mengi ya Kingereza. Makundi ya watu yaliyolengwa Walengwa wa kitabu hiki ni makundi ya watu yafuatayo: Watalii, wawekazeji wa kigeni na wafanyabiashara wanaotoka katika nchi zisizozungumza Kiswahili .Wafanyakazi katika Balozi zilizo katika nchi zinazozungumza Kiswahili .Walimu wa Shule za Awali na Msingi, wanafunzi wa Shule za Sekondari na Wanavyuo.
ThriftBooks sells millions of used books at the lowest everyday prices. We personally assess every book's quality and offer rare, out-of-print treasures. We deliver the joy of reading in recyclable packaging with free standard shipping on US orders over $20. ThriftBooks.com. Read more. Spend less.