Skip to content
Scan a barcode
Scan
Paperback Nyuso za Mwanamke [Swahili] Book

ISBN: 9966364455

ISBN13: 9789966364456

Nyuso za Mwanamke [Swahili]

Mwanamke kama dutu la udongo wa mfinyanzi huumbwa na kuumbuliwa

na jamii kwa namna mbalimbali. Kama kinyonga, uso wake unabeba rangi

tofauti tofauti kulingana na mikondo ya maisha na mapigo ya wakati.

Itakuwaje mwanamke awe wa kuozwa kama mwenye ugaga wa hisia za

kujichagulia mwenyewe; au awe wa kuuzwa kama pakacha la maembe

katika soko la umma? Uso wa mwanamke ni njia mbilimbili; ikiwa hazai

analea, asipokuwa akirembesha anarembeshwa, kama hatumbuizi

anatumbuizwa, ikiwa hajengi anabomoa; na kila mtu anamtazama na

kumtarajia aonyeshe uongofu wa malaika kama kwamba yeye si mtu.

Haya yanapokolea ndipo mwanamke anaonyesha nyuso zake.


Nana, msichana mrembo anajipata katikati ya jamii yenye mielekeo ya

kumfinyanga mwanamke na kumyumbisha kama kayamba. Kila

anayemwona Nana anamchukulia kuwa ni pambo la mji lenye nyuso

nyingi au lisilokuwa na uso hata mmoja. "...Bwana Hila... alidhani tu

maisha ya mwanamke ni kustareheshwa ...anachostahiki ni kupewa kila

kitu anachokitaka...apewe mawazi ya kifahari, manukato ghali, chakula

cha rutuba...mradi tu mwanamke abaki ndani kungoja kumstarehesha

bwana."


Anapotambua kuwa ana nyuso nyingi, Nana anajitazama kwa kioo kipya

na kuanza safari mpya.

Recommended

Format: Paperback

Temporarily Unavailable

We receive fewer than 1 copy every 6 months.

Save to List

Related Subjects

Fiction Literature & Fiction

Customer Reviews

0 rating
Copyright © 2026 Thriftbooks.com Terms of Use | Privacy Policy | Do Not Sell/Share My Personal Information | Cookie Policy | Cookie Preferences | Accessibility Statement
ThriftBooks ® and the ThriftBooks ® logo are registered trademarks of Thrift Books Global, LLC
GoDaddy Verified and Secured