"Mambo 15 Tunayokosea Wakati wa Kuomba", ni kitabu kinachoeleza makosa ambayo tumekuwa tukiyafanya wakati wa kuomba yanayosababisha maombi yetu yasijibiwe na Mungu Baba. Pia, kinaeleza utofauti uliopo kati ya sala na maombi; na kina shuhuda za kweli za watu waliojibiwa maombi yao kwa kutumia mbinu ambazo Mungu Baba anataka tuzitumie wakati wa kuomba. Hakuna mtu asiyekuwa na mahitaji ya kumuomba Mungu katika maisha yake. Tunaweza kudhani kwamba: watu wenye mali nyingi, kazi nzuri, elimu kubwa, vyeo au nyadhifa fulani; hawana shida katika maisha yao. Lakini ukweli ni kwamba, kila mtu ana shida au matatizo ambayo amekuwa akimuomba Mungu amuepushe nayo. Swali la kujiuliza hapa ni kwamba: kwa nini maombi yetu yanachelewa kujibiwa au hayajibiwi kabisa na Mungu Baba? Majibu ya maswali hayo utayapata ndani ya kitabu hiki kupitia siri zilizojificha katika Maandiko Matakatifu.
Format:Paperback
Language:Swahili
ISBN:B09V3YN1M7
ISBN13:9791092789171
Release Date:March 2022
Publisher:Diffusion Des Litteratures En Langues Africai
ThriftBooks sells millions of used books at the lowest everyday prices. We personally assess every book's quality and offer rare, out-of-print treasures. We deliver the joy of reading in recyclable packaging with free standard shipping on US orders over $20. ThriftBooks.com. Read more. Spend less.