Mfululizo huu wa Kazi za Christopher Mwashinga una lengo la kuwafikia wasomaji wa lugha ya Kiswahili kila mahali lugha ya hiyo adhimu inapotumika. Christopher R. Mwashinga alianza kuandika kazi mbalimbali kwa lugha ya Kiswahili mwanzoni mwa miaka ya 1980. Toleo hili la mfululizo wa kazi zake za Kiswahili, linahusisha mashairi, barua na maandiko yake mengine, ikiwa ni pamoja na kazi zake za kisomi na kitaaluma zilizowahi kuchapishwa kwa Kiswahili katika vitabu, magazeti, na majarida mbalimbali. Aidha mradi huu unahusisha pia kazi zake zilizotafsiriwa toka lugha ya Kiingereza. Miongoni mwa mambo mengine, maandiko yake yaliyowekwa katika majuzuu haya yamehifadhi maarifa na historia ya muhimu inayoihusu jamii yote kwa ujumla, na kwa namna ya kipekee, jamii ya Kikristo, hasa katika ukanda wa Afrika Mashariki. Baadhi ya mambo yaliyomo katika majuzuu haya, hayajarekodiwa mahali pengine popote katika historia ya watu wa Afrika Mashariki. Ukweli huu unafanya mfululizo huu wa machapisho yake uwe wa muhimu sana katika kazi za wenyeji wa Bara la Afrika zilizochapishwa katika miongo ya hivi karibuni. Juzuu hii ya tatu inahusisha mashairi yake yaliyoandikwa katika miongo miwili ya kwanza ya karne ya ishirini na moja (2001-2020). Mashairi haya yaliandikwa katika mabara manne: Afrika, Asia, Amerika ya Kaskazini na Ulaya.
ThriftBooks sells millions of used books at the lowest
everyday prices. We personally assess every book's quality and offer rare, out-of-print treasures. We
deliver the joy of reading in recyclable packaging with free standard shipping on US orders over $15.
ThriftBooks.com. Read more. Spend less.