Skip to content
Scan a barcode
Scan
Paperback Hujafa Hujaumbika [Swahili] Book

ISBN: 9966315683

ISBN13: 9789966315687

Hujafa Hujaumbika [Swahili]

Mwanga, almaarufu 'Fumo', ni kijana mdogo ambaye hana hakika na asili wala

fasili yake. Yeye ni msi baba, msi mama. Anachokifahamu ni kwamba

'aliokotwa' kutoka katika makao ya mayatima. Licha ya kuwa yeye ni kiokote,

mlezi wake anampa kila kinachostahili kwa mtoto mwenye wazazi wote.

Hali inapoonekana kutakata, msiba baada ya msiba unabisha. Mlezi wake wa

pekee ambaye anamjua kama 'mama' anapigwa kalamu. Nyumba yao inauzwa

kwa wenye nacho. 'Dada yake' Fumo ananajisiwa na kubaki hali mahututi

katika mshikemshike wa kufurushwa kutoka kwa nyumba yao na wahuni

walioletwa na mmiliki mpya. Baadaye, mlezi wa Mwanga anafunguliwa

mashtaka ya kusingiziwa ili asiweze kufuata kesi ya kufutwa au kufurushwa

kutoka kwa nyumba yake. Mwanga na 'familia' yake wanajipata katika mitaa

ya vitongoji duni. Choo ni cha 'kurusha fataki' na bafu ni upenuni. Hamna stara

tena!

Akiwa shuleni, Mwanga anafanya bidii ya mchwa na kupita vyema, lakini

mikosi bado haimwachi akapumua. Huku akicheza na watoto wengine,

anajipata amekanyaga kilipuzi na kupoteza mguu wake. Lakini bidii yake na

kudura za Mwenyezi Mungu vinamwezesha kuwa mwanasheria nguli. Azma

yake sasa ni kutetea haki licha ya kilema chake. Kumbe kufa si kufariki, kufa

ni kuoza utumbo!

Hii ni riwaya ya kusisimua yenye kutia matumaini katika jamii iliyotamauka

kutokana na matatizo mengi yanayoletwa na ufisadi na kupotoka kwa

maadili.

Recommended

Format: Paperback

Temporarily Unavailable

We receive fewer than 1 copy every 6 months.

Save to List

Related Subjects

Fiction Teen & Young Adult

Customer Reviews

0 rating
Copyright © 2026 Thriftbooks.com Terms of Use | Privacy Policy | Do Not Sell/Share My Personal Information | Cookie Policy | Cookie Preferences | Accessibility Statement
ThriftBooks ® and the ThriftBooks ® logo are registered trademarks of Thrift Books Global, LLC
GoDaddy Verified and Secured